Monday, October 31, 2011

JUMUIYA YA TEKNOLOJIA YA AFYA KULETA WATAALAMU ZANZIBAR

Washington DC:-
 
Jumuiya inayojishughulisha na Teknolojia ya Afya { MED } Nchini marekani inajipanga kuandaa ratiba ya Wataalamu wao wa afya kuja Zanzibar kusaidia huduma za afya katika Hospitali za Visiwani.
Mwakilishi wa jumuiya hiyo kutoka chuo Kikuu cha Brown Nchini Marekani Bwana jayson Marwaha ameeleza hayo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kwenye Ubalozi wa Tanzania Mjini Washington DC.
 
Bw. Jayson alisema Jumuiya yake imeshatenga kiasi cha Dolla za Kimarekani 14,000 kwa ajili ya kusaidia huduma za afya katika Vituo vya Afya vilivyomo vijijini kupitia shirika la misaada la Marekani US aid.
 
Bw. Jayson alimueleza Balozi Seif kwamba mpango huo utakaojumuisha huduma za  uchunguzi wa Virusi vya Ukimwi, huduma za watoto pamoja na mafunzo ya matumizi ya Vifaa vya kisasa utaanzia nchini Malawi.
Mwakilishi huyo wa MED alisema kwamba Taasisi yake itaendelea kuangalia maeneo ambayo inaweza ikaisaidia Zanzibar katika masuala ya Afya.
 
Mapema Naibu Waziri wa Afya Zanzibar Dr. Sira Ubwa Mamboya alimueleza Mwakilishi huyo wa Jumuiya inayojishughulishs na Teknolojia ya Afya kwamba Zanzibar imeweza kupiga hatua kubwa katika huduma za akina mama na watoto.Dr. Sira amesema kinachozingatiwa zaidi hivi sasa na serikali ni mipango ya kuziwezesha Hospitali za Mikoa kutoa huduma za lazima za afya ili kupunguza wimbi la wagonjwa katika Hospitali Kuu ya Manazi Mmoja.
 
Akitoa shukrani zake Mkamu wa Pili wa Ris wa Zanzibar balozi Seif Ameipongeza Taasisi hiyo kwa  juhudi zake za kuonyesha moyo wa kusaidia sekta ya afya Zanzibar.
Balozi Seif alisema hatua hiyo itakwenda sambamba na baadhi ya wataalamu wanaosaidia huduma za afya kutoka mashirika na nchi wahisani..
 
"Tumekuwa tukipokea Madaktari wa fani tofauti kutoka China na Cuba. Sasa kuwepo kwenu Zanzibar na nyinyi Mtasaidia kuongeza huduma za Afya kwa Wananchi walio wengi ". Alisema Balozi Seif.
 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
30/10/2011.

No comments:

Post a Comment